Jumanne 23.06.09 : Tanga - Wete
Kivuko kuelekea kisiwa cha Pemba kinaondoka mapema. |
Safari inadumu masaa nne na nusu na, bahati, watu wa daraja la kwanza (na la pili) wanaweza kutumia viti vya anasa kwa kupumzika |
Baada ya kufika Wete, tunapita ofisini ya uhamiaji ; wavulana wawili wanatupendekezea kwenda hotelini tuliyochagua (sisi na Lucie)
na tunafuatana kwa miguu. |
Noemie na Lucie wanakwenda kuogelea baharini na mimi ninatafuta ofisi ya mtandao na Beka ; inaonekana ofisi itafunguliwa kesho.
Halafu Beka ananipeleka katika nyumba ya mama anayetwanga muhogo na bibi wengine wanaangalia luninga.
Nyumba hiyo ni mkahawa pia na tunakunywa kinywaji ; kiongozi yangu ni mwislamu lakini anapenda sana gin !
Kisha tunakwenda kwake na ninaongea kidogo na mama yake na dada yake.
Baada ya kula vyakula vizuri, marafiki wetu wawili (Kassim na Beka) wanatuendesha mpaka mkahawani na tunaongea
sana kuhusu safari yetu ya kesho. |
yaliyomo