Jumanne 23.06.09 : Tanga - Wete
|
Kivuko kuelekea kisiwa cha Pemba kinaondoka mapema. |
|
Safari inadumu masaa nne na nusu na, bahati, watu wa daraja la kwanza (na la pili) wanaweza kutumia viti vya anasa kwa kupumzika |
|
|
Baada ya kufika Wete, tunapita ofisini ya uhamiaji ; wavulana wawili wanatupendekezea kwenda hotelini tuliyochagua (sisi na Lucie)
na tunafuatana kwa miguu. |
Noemie na Lucie wanakwenda kuogelea baharini na mimi ninatafuta ofisi ya mtandao na Beka ; inaonekana ofisi itafunguliwa kesho.
Halafu Beka ananipeleka katika nyumba ya mama anayetwanga muhogo na bibi wengine wanaangalia luninga.
Nyumba hiyo ni mkahawa pia na tunakunywa kinywaji ; kiongozi yangu ni mwislamu lakini anapenda sana gin !
Kisha tunakwenda kwake na ninaongea kidogo na mama yake na dada yake.
|
Baada ya kula vyakula vizuri, marafiki wetu wawili (Kassim na Beka) wanatuendesha mpaka mkahawani na tunaongea
sana kuhusu safari yetu ya kesho. |
|
yaliyomo
|
|
|