Jumapili 21.06.09 : Dar-es-Salaam



Leo, tunakwenda Msasani, kaskazini ya Dar-es-Salaam ; ni kitongoji cha matajiri na nyumba kubwa.
Tunapanda daladala kubwa kuliko daladala za Rwanda.
Tunateremka kuona sanaa ya mkoa inayoitwa Tinga-Tinga, tukanunua vyakula na tukaenda mwambaoni kufanya pikiniki kandokando ya bahari ya Hindi.
Wakazi wanaogelea baharini lakini hatuoni mzungu hata mmoja.

Ni picha ya duka la wasanii wa Msasani.

Hapa tunapanda bajaji (usafiri wa nchi) kwenda mwisho wa barabara.
Pale, kuna hoteli za watalii matajiri.
Tunaona wazungu mengi na waasia.
Tunakunywa kidogo na tunarudi Dar-es-Salaam.


Nimejua Noemie anasahau siku zote kitu kila mahali ; na sasa, anasahau kitabu cha kiongozi cha Tanzania katika daladala.
Ni kitabu muhimu kwani kinatusaidia siku zote.
Anakwenda kusubiri daladala hiyo itarudi tena katika kituo.
Dereva amekuta kitabu, akakiuza kwa mtu mwingine ndani ya daladala.
Tunaongea sana na dereva na mtu huyu : hatimaye tukakipewa tena.

Usiku huu, hotelini, ni sherehe ya mwanamke atafunga ndoa punde.
Tunaona desturi hiyo lakini kuna makelele mengi kwa sauti ya juu.

yaliyomo