Ijumaa 19.06.09 : Dar-es-Salaam


Kama ilivyokuwa Kigali, mwaka 2007, mwadhini anaanza kuimba saa kumi na moja alfajiri na kisha, kanisa katoliki karibu na hoteli linapiga kengele na kisha watu wa kanisa wanaimba kwa sauti kama ndege.
Leo, tunazunguka kwa miguu katika Dar-es-Salaam yote.
Mchana, tunakwenda mpaka mwisho wa mto na tunaelekea soko la samaki.

Inanuka sana !
Mbele, watu wengine wanaonyesha dagaa zao na nyuma, bibi wanaketi juu ya ndoo na wananunua samaki

Ninaongea na vijana wauzaji wa samaki na tunacheka sote pamoja. Wanakubali ninawapiga picha na wananipa anwani ya kuwafikishia picha.
Baada ya kuzumgunza mambo mbalimbali, tunaondoka kutembelea soko la matunda na mboga.
Kisha, tunaamua kupanda kivuko kuelekea Kigamboni.

Unaweza kuona picha ya kuwasili Kigamboni, kutoka ndani ya kivuko ; mwendo yapata dakika kumi
Hapa ni tofauti sana : kuna maduka mengi na hasa maduka ya machungwa ya kupapatuwa. Maganda yametapakaa chini na chupa za plastiki, n.k.
Kila mahali, kuna watoto wazuri, wema sana na maridadi

Baada ya chakula cha usiku, ninangoja mzigo ambao karani wa uwanja wa ndege aliahidi kuniletea leo. Msichana wa hoteli ananiambia kuwa ataniwekea mzigo ili niweze kulala sasa.


yaliyomo